Mimba na ndoa za utotoni kupingwa kwa marathoni Jumapili
Nchini Tanzania Jumapili hii kutafanyika mbio za kimataifa za marathoni za Kilimanjaro Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu, UNFPA itatumia mbio hizo kueneza ujumbe wa kupinga mimba na ndoa za utotoni.
Katika mahojiano Afisa wa UNFPA Sawiche Wamunza amemweleza Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini humo kuwa hii ni mara ya pili wanadhamini mbio hizo na wanaamini ni njia muhimu ya kuwafikia vijana kwenye nchi hiyo ambayo asilimia 23 ya wasichana wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 19 wamepata watoto wakiwa na umri mdogo.
(Sauti ya Sawiche)