Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatimaye wakimbizi wa Somalia walioko Kenya kuanza kurudishwa makwao kwa hiari

Hatimaye wakimbizi wa Somalia walioko Kenya kuanza kurudishwa makwao kwa hiari

Waswahili husema dalili za mvua ni mawingu, na panapofuka moshi kuna moto. Hii ni misemo inayoweza kuitumika kuelezea matumaini ya kutekelezeka kwa mkataba wa kuwarejesha makwao kwa hiari wafungwa wa Somalia waliko nchini Kenya zoezi ambalo awali lilikwama.

Katika mahojiano maalum na Joseph Msami wa idhaa hii msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi UNHCR nchini Kenya Abel Mbilinyi ambaye pia anaeleza namna Kenya inavyowahifadhi wakimbizi wa Sudani Kusini, amesema ziara ya waziri mkuu mpya wa Somalia nchini humo imefufua matumaini kw awakimbizi wan chi hiyo matumaini ambayo yalififia kutokana na uwepo wa serkali mpya nchini humo.

(SAUTI MAHOJIANO)