Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uwezo wa kusoma bado ni ndoto kwa wengi

Uwezo wa kusoma bado ni ndoto kwa wengi

Hivi karibuni shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO lilichapisha taarifa iliyoanisha hali ya elimu ya msingi duniani ambapo pamoja na mambo mengine ripoti hiyo inaonyesha kuwa kati ya vijana wanne mmoja hajui kusoma duniani kutokana na ukweli kwamba elimu hiyo ya msingi haijatekelezwa kwa nchi nyingi kama inavyopaswa.

Noel Thomson wa radio washirika Afrya radio ya Mwanza Tanzania amefuatilia suala hilo na kuandaa taarifa ifuatayo.