Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tanzania,Australia kuongoza mjadala siku ya radio duniani.

Tanzania,Australia kuongoza mjadala siku ya radio duniani.

Tukiwa tunaelekea siku ya radio duniani tarehe 13 mwezi huu, mratibu wa siku hiyo katika radio ya Umoja wa Mataifa Flora Nducha amesema mjadala maalum utakaoratibiwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO utafanyika katika makao makuu ya Umoja huo mjini New York huku pia akisema Tanzania na Australia zitakuwa kinara katika mjadala huo kuhusu namna radio inavyowezesha wanawake na wasichana.

Akihojiwa na Joseph Msami wa Idhaa hii Bi Nducha anaanza kueleza nini wasikilizaji watarajie katika kuadhimisha siku ya radio duniani.