Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjukuu wa Mandela aeleza babu yake alivyomfunda

Mjukuu wa Mandela aeleza babu yake alivyomfunda

Nelson Mandela, ametutoka lakini uwepo wake utaendelea kuwa dhahiri . Hilo limedhihirika baada ya mjukuu wake Ndaba Mandela kuzindua kampeni ya Linda Lango iliyoko chini ya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Ukimwi UNAIDS ambapo Ndaba ni msemji wa kampeni hiyo inayotumia michezo kuhamasisha jamii hususani vijana.

Katika mahojiano maaluma na Joseph Msami wa idhaa hii Ndaba anaanza kwa kujibu swali kwanini aliamua kujihusisha na masuala ya michezo katika kuhamasisha amani na maendeleo?