Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi wa Sudan Kusini wamiminika Kenya na Uganda

Wakimbizi wa Sudan Kusini wamiminika Kenya na Uganda

Mapigano nchini Sudan Kusini yamesababisha wimbi jipya la wakimbizi wanaowasili katika nchi jirani kutafuta usalama. Kwa mujibu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, Kambi ya Kakuma Kaskazini Mashariki mwa Kenya imekuwa ikipokea wakimbizi wapatao 300 kila siku, huku idadi ya wakimbizi wanaowasili nchini Uganda kwenye kambi ya Kiryandongo ikiwa imepanda pia. John Kibego wa Redio washirika ya Spice FM yupo kwenye kambi hiyo na amefanya mahojiano maaluma na Joseph Msami kuhusu kile anachokiona kamabini hapo.

(Sauti Maojiano)