Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MONUSCO yatoa usaidizi kwa wapiganaji waliojisalimisha DRC

MONUSCO yatoa usaidizi kwa wapiganaji waliojisalimisha DRC

Zoezi la usaidizi kwa wapiganaji wanaojisalimisha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC linaendelea ambapo wapiganaji hao wanajumuishwa katika jamii huku wengine wakijumuishwa katika jeshi la serikali kwa hiari.

Joseph Msami anamulika zoezi hili huko mashariki mwa DRC katika makala inayoangazia namna ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC unavyosaidia kuweka utulivu katika nchi hiyo iliyokumbwa na mizozo kwa miongo kadhaa.