Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watoto milioni 230 duniani hawajasajiliwa:UNICEF

Watoto milioni 230 duniani hawajasajiliwa:UNICEF

Mada ya usajili kwa watoto wanaozaliwa imekuwa muhimu kufuatia ripoti ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF ya kwamba watoto Milioni 230 duniani kote hawajasajiliwa popote. Sababu zimetajwa kuwa ni pamoja na ukosefu wa mfumo wa kuhakikisha mtoto anapozaliwa anasajiliwa na kupatiwa cheti cha kuzaliwa. Sababu nyingine ni uhusiano wa kijinsia ambapo wanawake ambao wanakuwa wanalea ujauzito peke yao baada ya kukataliwa na waume zao wanashindwa kusajili watoto wao kwani hawezi kutumia jina la ukoo wake. Nchini Tanzania yaelezwa kuwa hatua zimechukuliwa kuhakikisha watoto wanasajiliwa ili waweze kupata haki zao za msingi kwa usahihi. Je hali ikoje? Basi ungana na Tamimu Adamu wa Radio washirika Jogoo FM kutoka Ruvuma nchini Tanzania.

(PKG YA TAMIMU ADAMU)