Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashirika ya UM yazindua mpango wa kuokoa chakula

Mashirika ya UM yazindua mpango wa kuokoa chakula

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayohusika na chakula yamezindua mpango wa pamoja wenye shabaha ya kukabiliana na tatizo la upotevu wa chakula duniani. George Njogopa na taarifa zaidi.

(Taarifa ya George)

Yote kwa pamoja, mashirika hayo lile la mpango wa chakula duniani WFP, Shirika la chakula na kilimo FAO na fuko la kimataifa la maendeleo ya kilimo IFAD yamedhamiria kutokomeza tatizo la upotevu wa chakula.

 Inakadiriwa kuwa,theluthi moja ya chakula kinachozalishwa kwa ajili ya ulaji wa binadamu kinapotea kila mwaka ikiwa ni wastani wa tani billion1.3. Kiasi hicho cha chakula kinachopotea kina uwezo wa kulisha watu bilioni 2.

Mpango huo ambao unagharimu dola za Marekani milioni 2.7 unatazamiwa kutekelezwa katika nchi tatu barani Afrika.Nchi hizo ni Burkina Faso, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Uganda