Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Miaka 50 ya uhuru wa Kenya yaenziwa New York

Miaka 50 ya uhuru wa Kenya yaenziwa New York

Taifa la Kenya limetimiza miaka 5o tangu lijipatie uhuru wake kutoka kwa wakoloni ,Uingereza. Sherehe za kitaifa zimefanyika nchini humo ambapo wananchi wa taifa hilo lililoko Mashariki mwa Afrika waliadhimisha sherehe hizo kwa mambo kadhaa ikiwamo mkesha maalum ulioshuhudia kupandisha tena bendera ya Kenya kitendo kilichofanyika baada ya kuishusha ya mkoloni.

Hapa mjini New York katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa raia wa Kenya wanaoishi hapa wameungana na jamii mbalimbali katika kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wao huku pia wakiadhimisha miaka 50 tangu kuasisi uwakilishi wao katika Umoja wa Mataifa. Grace Kaneiya amekuwa shuhuda katika sherehe hiyo na kuandaa makala ifuatayo

(Makala ya Grace)