WFP yasambaza mafuta kwa Wasyria kunapoanza msimu wa baridi
Huku watu nchini Syria wakikabiliana na msimu wa baridi kali shirika la mpango wa chakula duniani WFP limeanza shughuli za usambazaji wa karibu tani 10,000 za mafuta kwa wakimbizi wa ndani wanaoishi kwenye maeneo kumi ya mji wa Damascus.
Mafuta yanayosambaza nayo yatatumika kwenye upishi na kwa kupasha joto. Usambazaji zaidi wa mafuta unapangwa kufanywa kwenye sehemu 35 za mji wa Homs, Hama na vitongoji vya mji wa Damascus siku zinazokuja.
WFP imesambaza migao 3000 ya chakula kinachoweza kulisha watu 15,000 kwa kipindi cha mwezi mmoja ikiwa pia na mpango wa kutoa chakula kwa watu milioni 4 mwezi huu kote nchini Syria.
Makundi ya kutoa misaada hayajafanikiwa kufika eneo la Al Hassakeh kwa muda wa miezi mitano iliyopita kutokana na kuwepo ukosefu wa usalama barabarani.