Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

AMISOM yaahidi kulinda haki za watu Somalia

AMISOM yaahidi kulinda haki za watu Somalia

Mjumbe maalumu wa mwenyekiti wa kamishna ya Afrika kwa Somalia amerejelea wito wa kuendelea kuinga mkono taifahilo laSomalia katika wakati ambapo dunia ikiadhimisha siku ya haki za binadamu.

Akizungumza sambamba na maadhimisho ya siku hiyo Balozi Mahamat Saleh Annadif amesema kuwa ujumbe wa kimatafa nchini Somalia AMISON umedhamiria kuendelea kuisadia Somalia na kutetea haki za watu wake.

Amesema kuwa AMISON itaendelea kufanya kazi bega kwa began a serikali ya shirikisho kwa shabaha ya kuleta usawa na kuwajengea uwezo wale waliotengwa na kukosa fursa.

Balozi huyo ameongeza kuwa, vikosi vya AMISON vimepokea mafunzo ya ziada yatayosaidia kuboresha mifumo ya utoaji wa huduma nchini humo.