Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uhaba wa vyoo wahatarisha afya za wananchi nchini Kenya

Uhaba wa vyoo wahatarisha afya za wananchi nchini Kenya

Dunia ikiadhimisha siku ya choo duniani leo Nov 19, 2013 baadhi ya nyumba bado hazina vyoo. Takwimu zinaonyesha kuwa watu zaidi ya bilioni 2.5 kote duniani hawana vyoo hatua inayoweza kusababisha matatizo ya afya kwao. Mwandishi wetu Jasson Nyakundi anamulika hali ilivyo nchini Kenya ambapo anazungumza na Samwel Waweru akiwa Mukuru Kwa njenga anayemiliki choo cha biashara.