Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuwafikia wakimbizi wa kipalestina huko Yarmouk bado ni taabu: UNRWA

Kuwafikia wakimbizi wa kipalestina huko Yarmouk bado ni taabu: UNRWA

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na usimamizi na huduma kwa wakimbizi wa kipalestina, UNRWA linazidi kupata hofu juu ya hatma ya wakimbizi hao hususan walioko kambi ya Yarmanouk kwa kuwa hivi sasa hawawezi kufikiwa ili kupatiwa huduma muhimu.

Taarifa ya UNRWA inasema wakimbizi hao wanahitaji misaada ya kibinadamu lakini kutokana na hofu ya usalama watoa huduma wanashindwa kufika. Shirika hilo linasema serikali ya Syria na pande zote husika zina mamlaka za kuwezesha UNRWA kusambaza misaada hiyo kwa usalama ili kupunguza madhila yanayokabili wakimbizi wa kipalestina. Kwa mujibu wa UNRWA tangu mwezi Julai mwaka huu licha ya maombi na jitihada kadhaa, wakimbizi wa kipalestina huko

Yarmanouk wamekuwa wakikabiliwa na fursa ndogo zaidi ya uhuru wa kutembea na hata kupata misaada ya kibinadamu.