Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahudumu wa Afya wametia nanga Ufilipino: WHO

Wahudumu wa Afya wametia nanga Ufilipino: WHO

Nchini Ufilipino zaidi ya wiki moja baada ya kimbunga Haiyan kupiga eneo hilo, Shirika la afya duniani WHO linasema timu ya wataalamu wa afya inayofuatilia magonjwa iko nchini humo ijapokuwa hakuna mlipuko wa magonjwa uliokwisharipotiwa. Jason Nyakundi na Ripoti kamili.

(Ripoti ya Jason)

Mengi ya makao 1500 kwenye maeneo yaliyokumbwa na kimbuga yana misongamano ya watu na kuna hofu kuwa huenda kukatokea mikurupuko ya magonjwa.

WHO inasema kuwa usambazaji wa madawa unaendelea lakini bidhaa zaidi zinahitajika. Idara ya afya nchini Ufilipino inaendesha kampeni ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Surua na Polio kwenye maeneo yaliyoathirika.

Msemaji wa WHO Tarik Jasarevice ameiambia Radio ya Umoja wa Mataifa kuwa WHO inasaidia kurejesha huduma za vituo vya afya kwenye sehemu zizizoathiriwa.

(Sauti ya Tarik)