Mchezo wa baiskeli ni mtaji wa mshikamano Rwanda
Rwanda, taifa ambalo lilitatizika kwa mauaji ya halaiki takribani miaka 20 iliyopita, sasa liko katika mchakato wa utangamano. Hatua hii jumuishi inahitaji sekta zote kuwajibika, na hii ndio sababu ya kuanzisha mchezo wa basikeli wenye lengo la kuwaweka vijana na kamundi mbalimbali pamoja bila kujali tofauti zao.
Ungana na Joseph msami katika makala inayomulika filamu iitwayo Amka majivuni ambayo kwayo utafahamu jinsi mchezo wa baiskeli ulivyotumika kuhamasisha umoja na mashikamano nchini humo.