Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Viongozi wa dini Uganda shawishini wajawazito waende kliniki: Dkt. Rugunda

Viongozi wa dini Uganda shawishini wajawazito waende kliniki: Dkt. Rugunda

Nchini Uganda harakati zinaendelea kufikia lengo namba Tano la Milenia la kupunguza vifo vya wajawazito ambapo Waziri wa Afya amewatolea wito viongozi wa kidini kuhimiza wajawazito kwenda kliniki. Inaelezwa kuwa idadi ya wajawazito wanaofarikidunia wakati wa kujifungua, ilishuka kutoka 435 hadi 310 kwa kila wajawazito laki moja mwaka 2010 lakini ripoti mpya nchini Uganda inaonyesha kuwa vifo hivyo vimepanda upya hadi 438.John Kibego wa radio washirika ya Spice FM hukoUganda ameandaa tarifa ifatayo.

(Taarifa ya John Kibego)

Akiongea kwenye uzinduzi wa jengo la kitengo cha kusajili wagonjwa wapya kwenye kituo cha afia cha Azur mjini Hoima, waziri wa afia Dr. Ruhakana Rugunda amesema, ni jambo la kuaibisha Uganda kubaakia nyuma katika vita dhidi ya vifo vya wajawazito. Kwa mujibu wake, vifo vingi vinngeliweza kuzuilika kwa vile sababu zake zinajulikana.

(Sauti ya Dr. Ruhakana Rugunda)