Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usalama na ulinzi wazorota CAR na DR Kongo

Usalama na ulinzi wazorota CAR na DR Kongo

Hofu kubwa imetanda nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati kufuatia mapigano ya vikundi vyenye silaha na kuitaka serikali ya mpito kuingilia katika kuimarisha usalama huku hali ya misaada ya kibinadamu ikiendelea kuzorota nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, DRC.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini new York Mkurugenzi wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaadaya kibinadamu John Ging ambaye hivi karibuni akiambatana na timu ya misaada ya kibinadamu amefanya ziara katika nchi hizo zenye migogoro, amesema nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, jamii ina hofu huku zaidi ya nusu ya watu wakihitaji misaada ya kibinadamu wakati huu ambapo mapigano bado yanaendelea

(Sauti Ging)

Kuhusu hali inavyozidi kuzorota huko DR Kongo Mkuu wa OCHA anasema ulinzi na usalama kwa wananchi bado ni changamoto kubwa lakini liko tumaini kwa jamii.

(Sauti Ging)