Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNMISS imelaani vikali mashambulizi jimboni Jonglei

UNMISS imelaani vikali mashambulizi jimboni Jonglei

Mpango wa Umoja wa Mataifa Sudan Kusini (UNMISS) umelaani vikali mashambulio dhidi ya raia siku ya Jumapili kwenye eneo la Twic Mashariki jimboni Jonglei. Mashambulio hayo yamesababisha idadi kubwa ya vifo na majeruhi.

Moja ya mashambulio hayo yamefanyika katika kambi za ng’ombe moja Paliau , huko Ajong Payam na lingine Maar huko Pakeer Payam, na mashambulio kadhaa katika maeneo mbalimbali. Baada ya mapigano kusita Jumapili humama za usafiri wa anga za Umoja wa Mataifa UNHAS iliwasafirisha wahudumu wa afya kwenye maeneo ya mashambulizi ili kuwaokoa manusura.

Hadi mwisho wa siku UNHAS imesafirisha watu 31 waliojeruhiwa vibaya sana kuwapeleka Bor na Juba na kuarifu kwamba majeruhi wengine zaidi ambao ni raia bado wapo kwenye eneo hilo na UNHAS imetuma helkopta kuendelea kuwahamisha.