Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano juu ya mkataba wa Minamata kufanyika Japan

Mkutano juu ya mkataba wa Minamata kufanyika Japan

Pande zinazohusika na mkutano wa kimataifa ujulikanao kama “ mkataba wa Minamata juu ya madini ya Zebaki” unatazamiwa kufanyika huko Minamata na Kumamoto nchini Japan kuanzia Octoba 9 hadi 11 mwaka huu.

Madini ya Zebaki ni moja ya zingatio kubwa na jumuiya ya kimataifa kutokana na kile kianchosemwa kwamba kemikali zake huzusha kitosho cha dunia kwani inaposafirishwa kwa umbali mrefu inaweza kuhaeribu mazingira ya dunia.

Zebaki inatajwa kuwa na mathari makubwa kuanzia mazingira ya dunia na maisha jumla ya binadamu.

Kemikali hizo zinaweza kuleta madhara makubwa kwa afya ya binadamu ikiwemo uwezekano wa kuharibu mimba .Tangu mwaka 2003, shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP limekuwa likiendesha kampeni ya matumizi ya kemikali hizo.