Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Malaysia yataka suluhu jumuishi la kisiasa kwa mzozo wa Syria

Malaysia yataka suluhu jumuishi la kisiasa kwa mzozo wa Syria

Normal

0

false

false

false

MicrosoftInternetExplorer4

st1\:*{behavior:url(#ieooui) }

/* Style Definitions */

table.MsoNormalTable

{mso-style-name:"Table Normal";

mso-tstyle-rowband-size:0;

mso-tstyle-colband-size:0;

mso-style-noshow:yes;

mso-style-parent:"";

mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;

mso-para-margin:0in;

mso-para-margin-bottom:.0001pt;

mso-pagination:widow-orphan;

font-size:10.0pt;

font-family:"Times New Roman";

mso-ansi-language:#0400;

mso-fareast-language:#0400;

mso-bidi-language:#0400;}

Malaysia imetoa wito kuwepo suluhu la kisiasa kupitia harakati zinazowajumuisha wote nchini Syria.

Akitoa hotuba yake wakati wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Waziri Kuu wa Malaysia, Mohd Najib Tun Abdul Razak, amesema taifa la Malaysia linapinga hatua yoyote isowajumuisha wote katika kuutatua mzozo wa Syria. Amesisitiza kuwa pande zote ni lazima zije pamoja na kutafuta suluhu la kisiasa.

Tunakaribisha makubaliano ya mkakati ulioongozwa na Marekani na Urusi, tunalaani vikali matumizi ya silaha za kemikali, na kutoa wito kwa jamii ya kimataifa kuongeza juhudi za kutafuta njia za kidiplomasia za kuleta amani chini ya Umoja wa Mataifa. Ni lazima pia tutafute mtazamo na nia ya kisiasa ya kutafuta suluhu la haki kwa ajili ya Palestina. Tunatataraji kuwa hatua za kupatikana taifa huru la Palestina, kutokana na mipaka ya kabla ya mwaka 1967, na Jerusalem Mashariki kama mji mkuu, zitafanywa.

Waziri huyo Mkuu wa Malaysia ameelezea matumaini yake kuwa Marekani na wanachama wengine wa nchi nne husika wataendelea kutoa mchango wao kama wapatanishi wa kuaminika katika harakati hizo. Amesisitiza kuwa ni kupitia katika amani tu ndipo kutakuwepo maendeleo na utu kwa watu wa Palestina.