Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Biashara ya hewa ya ukaa bado kitendawili, gesi chafuzi zinazidi na umaskini ni kikwazo: Tanzania

Biashara ya hewa ya ukaa bado kitendawili, gesi chafuzi zinazidi na umaskini ni kikwazo: Tanzania

Tanzania inaendelea na jitihada za kupunguza makali yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi wakati huu ambapo jopo la kimataifa la Umoja wa Mataifa linalojadili mabadiliko ya hali ya hewa IPCC limetoa ripoti kwamba shughuli za binadamu ndio chanzo kikuu cha mabadiliko hayo. Je Tanzania imefikia wapi? Na vipi biashara ya hewa ya ukaa?

Hayo na mengineyo aliulizwa Waziri husika wa mazingira wa Tanzania Dkt. Tereziya Huviza katika mahojiano maalum na Assumpta Massoi wa Radio ya Umoja wa Mataifa mjini New York.