Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban asikitishwa na ripoti mpya kuhusu mabadiliko ya tabianchi

Ban asikitishwa na ripoti mpya kuhusu mabadiliko ya tabianchi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon, amekaribisha ripoti ya tathmini ya tano ya jopo la kiserikali kuhusu mabadiliko ya tabianchi, IPCC na kusikitishwa na matokeo yake.

Ripoti hiyo inaweka dhahiri kuwa madhara anayosababisha mwanadamu kwenye mfumo wa tabianchi ni bayana katika maeneo mengi ya dunia, na inawezekana kuwa madhara hayo alosababisha mwanadamu yamekuwa ndiyo makubwa zaidi kwa ongezeko la joto duniani tangu kati mwa karne ya 20.

Bwana Ban amesema kupunguza mabadiliko ya tabianchi kutahitaji kupunguza kwa kiasi kikubwa gesi chafuzi za greenhouse na kwa njia endelevu. Katibu Mkuu ametoa wito kwa nchi zote kufanya kila juhudi inayohitajika ili kufikia mkataba wa kimataifa wa sheria kuhusu hali ya anga ifikapo mwaka 2015, na kuchukuwa hatua haraka kupunguza athari zake.