Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatua za kijeshi zinawaweza kuchokea hali kuwa mbaya Syria:Pillay

Hatua za kijeshi zinawaweza kuchokea hali kuwa mbaya Syria:Pillay

Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Navi Pillay amesema hatua za kijeshi kutoka nje au kuyapa silaha makundi ya waasi haiwezi kuleta amani nchini Syria.Jason Nyakundi anaaarifu

(PKG YA JASON NYAKUNDI)

Akihutubia baraza la haki za binmadamu la Umoja wa Mataifa Pillay amesema kuwa mateso wanayopitia wananchi wa Syria yamefikia viwango vya kutisha akiongeza kuwa hatua za kijsehi au kuendelea kuwapa silaha wanamgambo huenda vikasababisha maafa zaidi na pia mateso. Pillay amesema kuwa hakuna shaka kuwa silaha za kemikali zilitumika nchini Syria hata kama bado aliyehusika hajulikani. Pillay ameyataka mataifa yenye ushawishi kushirikina na Umoja wa Mataifa kwa haraka ili kutafuta njia ya kuzitea pande husika kwenye mazungumzo ili kuzuia umwagaji damu.

(SAUTI YA NAVI PILLAY)

Pillay pia amesema kuwa anaendela kushangazwa na ghasia zinazoendela nchini Misri naIraqna dhuluma zinazondeshwa dhidi  watetesi wa haki za binadamu nchiniBahrain