Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Naibu Katibu Mkuu wa UM asisitiza haja ya juhudi binafsi kuchagiza amani:

Naibu Katibu Mkuu wa UM asisitiza haja ya juhudi binafsi kuchagiza amani:

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Jan Eliasson amesisitiza umuhimu wa kuzungumzia juhudi binafsi katika kuchagiza utamaduni wa amani. 

Ameuambia mjadala wa Baraza Kuu kuhusu utamaduni wa amani kwamba Umoja wa Mataifa umeanzishwa kwa misingi ya utu na uzito wa kila binadamu, lakini kila wakati kunakuwa na ukiukaji wa misingi hii.

Bwana Eliasson amesema nchini Syria vita vya wenyewe kwa wenyewe vimekatili maisha ya watu zaidi ya 100,000 na kuwafanya theluthi moja kuwa wakimbizi wa ndani na nje huku vikichagiza mivutano ya kidini na kikabila ndani na nje ya nchi.

 (SAUTI YA ELIASSON)