Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Leo ni siku ya kimataifa ya masuala ya hisani

Leo ni siku ya kimataifa ya masuala ya hisani

Masuala ya hisani yana jukumu kubwa katika kuendeleza kazi za Umoja wa mataifa amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon .

Katika ujumbe maalumu ya maadhimisho haya ya kwanza Ban amesema kujitolea wakati au fedha , kushiriki katika shughuli za kijamii au za sehemu nyingine duniani , kufanya vitendo vya kusaidia na utu wema bila dhamira ya kulipwa , vitendo hivyo na vinginevyo vya kuonyesha mshikamano vinausaidia saana Umoja wa mataifa .

Ameongeza kuwa pia vinasaidia nia ya kuishi pamoja kwa mshikamano na kujenga mustakhbali wa amani kwa wote. Amewapongeza wote ambao wanatumia muda wao au fedha zao kwa ajili ya kutekeleza masuala ya hisani.