IOM yaendesha mafunzo ya kukomesha usafirishaji wa binadamu Kusini mwa Amerika
Katika juhudi za kukomesha biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu Amerika Kusini Shirika la kimataifa la Uhamiaji , IOM linaendesha mafunzo kwa askari, waendesha mashtaka na majaji kutoka nchi tisa juu ya uchunguzi wa biashara hiyo. Mafunzo hayo ya siku nne yanafanyika mjini Buenos Aires, Argentina na yameandaliwa kwa ushirikiano kati ya IOM, mtandao wa kimataifa wa polisi wa kupamabana na uhalifu (INTERPOL), na ofisi ya Umoja wa Matifa ya kupamabana na madawa ya kulevya na uhalifu. Jumbe Omari Jumbe ni msemaji wa IOM na hapa anafafanua zaidi.
(Sauti ya Jumbe)