Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jopo la UM la kuchunguza madai ya matumizi ya silaha za kemikali Syria, lawasili Damascus

Jopo la UM la kuchunguza madai ya matumizi ya silaha za kemikali Syria, lawasili Damascus

Ofisi ya msemaji wa Umoja wa Mataifa imearifu ya kwamba jopo lililoundwa na Katibu Mkuu Ban Ki Moon kuchunguza madai ya matumizi ya silaha za kemikali nchini Syria limewasili mjini Damascus Jumapili. Jopo hilo linaloongozwa na Profesa Ǻke Sellström, litaanza kazi yake Jumatatu tarehe 19. kwa mujibu wa taarifa ya leo, maelezo zaidi yatakuwa yanatolewa mjini New York kadri taarifa zitakavyokuwa zikipatikana. Tarehe 15 mwezi huu wa Agosti, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alitangaza kuwa serikali ya Syria  imekubali rasmi kutoa ushirikiano kuwezesha timu ya waangalizi kuendesha majukumu yake katika mazingira safi, salama na katika hali ya ufanisi.