FAO yazindua vitabu vyake vya kwanza vya mtandao
Shirika la kilimo na mazao la Umoja wa Mataifa FAO limezindua vitabu vyake vya kwanza vya mtandao vinavyoanganzia masuala kadha kuhusu chakula , kilimo na vita dhidi ya njaa. Jason Nyakundi anaripoti(RIPOTI YA JASON NYAKUNDI)
Kwa sasa nakala za kwanza za vitabu hivyo vinapatikana bila malipo kwenye wavuti wa Shirika la FAO. Nakala zingine zaidi zinatarajiwa kuwekwa kwenye mtandao kwenye awamu ambayo itaendela hadi baadaye mwaka huu kabla ya vitabu hivyo kuanza kupatika kwenye hifadhi zingine za vitabu.
Naibu mkuu kwenye kitengo cha uchapishaji katika Shirika la FAO Rachel Tucker anasema kuwa vitabu hivyo vikiwa vinaangazia masuala teule kwa njia ya mtandao ni hatua iliyo muhimu.
Anasema kuwa FAO ina habari nyingi kuhusu chakula, kilimo na njia za kupambana na njaa yote ambayo yatapatikana kwa urahisi kwa wale wanaoyahitaji. Vitabu hivyo vyote vianapatikana kwa lugha ya kiingereza.