Mashirika ya kutoa misaada yaongeza huduma zake eneo la Pibor
Wakati hayo yakijiri makundi ya vijana waliojihami wamekabiliana kwenye maeneo tofauti ya nchi . Zaidi ya majeruhi 200 kwenye makabiliano hayo wamesafirishwa kupewa matibabu na ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS. Umoja wa Mataifa kupitia huduma zake za anga pamoja na shirika la afya duniani WHO wanakagua eneo la Menyapol ili kuweza kuwasafirisha wale waliojeruhiwa zaidi kwenda Bor ambapo watapewa matibabu.