Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Elimu bado changamoto kwa wafugaji: Lowassa

Elimu bado changamoto kwa wafugaji: Lowassa

Siku chache baada ya Umoja wa Mataifa kutangaza July 12 kuwa siku ya Malala duniani ambapo elimu kwa mtoto wa kike itaangaziwa, Waziri Mkuu ms

taafu wa Tanzania Edward Lowassa amesema bado elimu ya mtoto wa kike ni changamoto nchini humo hususani kwa jamii ya wafugaji.

Katika mahojiano maalum na idhaa ya Kiswahili ya radio ya Umoja wa Mataifa mjini New York Lowasa amesema ziko juhudi zilizofanywa ambazo zinahitaji kuungwa mkono ili kutimiza lengo kabla ya ukomo wa maendeleo ya milenia mwaka 2015.

(SAUTI YA LOWASA)

Katika hatua nyingine kiongozi huyo mstaafu wa Tanzania amezungumzia nafasi ya wazee katika mpango wa maendeleoa baada ya 2015

(SAUTI YA LOWASA)

Mahojiano kwa urefu na mwanasiasa huyo yatapatikana katika ukurasa wetu.