Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Juhudi za amani zawakutanisha viongozi wa vikosi mbali mbali

Juhudi za amani zawakutanisha viongozi wa vikosi mbali mbali

Umoja wa Mataifa unaendelea kujitahidi kuboresha huduma za ulinzi wa amani, ili kuhakikisha ulinzi bora wa raia katika maeneo yaloathirika na mizozo.Ni katika hali hiyo ndipo wakuu wa vikosi mbalimbali vya kulinda amani wamekutana kwenye makao makuu ya Umoja huo mjini New York, ili kubadilishana mawazo kuhusu shughuli za ulinzi wa amani.

Mmoja wa makamanda hao ni Luteni Jenerali Paul Ignus Mela, kamanda mpya wa vikosi vya pamoja wa Muungano wa Afrika na Umoja wa Mataifa vya kulinda amani katika eneo la Darfur nchini Sudan, UNAMID, ambaye amezungumza na Joshua Mmali, kwanza kwa kumueleza wadhfa wake mpya unahusisha nini.

(SAUTI)