Kampeni ya chanjo ya polio Burundi baada ya tishio kutoka DRC
Serikali ya Burundi kwa ushirikiano na shirika la Afya Duniani WHO wameanzisha kampeni kabambe dhidi ya ugonjwa wa kupooza wa polio.
Hii ni baada ya Burundi kujikuta katika kitisho kikubwa cha kuvamiwa na maradhi hayo baada ya nchi jirani ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuonyesha dalili za Polio katika maeneo ya kusini na mashariki mwa nchi hiyo.
Watoto zaidi ya Milioni 1 na Laki 2 wanahusishwa na kampeni ambayo pia Shirika la WHO limepania kuineza katika maeneo mbalimbali ya DR Congo.
Kutoka Bujumbura, Muandishi wetu wa maziwa makuu Ramadhani KIBUGA ametuandalia makala hii.
(Makala ya Kibuga Ramadhani)