Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban alaani mashambulizi dhidi ya wanafunzi wa kike nchini Pakistan

Ban alaani mashambulizi dhidi ya wanafunzi wa kike nchini Pakistan

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amelaani mashambulizi yaliyolenga basi moja, hospitali na jumba la kihistoria nchini Pakistan ambapo watu 20 waliuawa wengi wakiwa ni wanafunzi wa kike. Kwenye taarifa kupitia kwa msemaji wake Ban amesema kuwa  ghasia dhidi ya wanawake zimeongezeka miaka ya hivi karibuni zikiwa na lengo la kuwazuia wasichana wasihudhurie masomo. Kulingana na ripoti za vyombo vya habari bomu lililokuwa limefichwa kweye basi iliyokuwa ikiwasafirisha wanafunzi wa kike lililipuka kwenye mji waQuettana baadaye watu waliokuwa wamejihami wakavamia hospitali ambapo waathiriwa walikuwa wamepelekwa . Jumla ya watu ishirini waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.