Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umoja wa mataifa una wasiwasi na ukiukwaji wa haki za binadamu Sudan Kusini

Umoja wa mataifa una wasiwasi na ukiukwaji wa haki za binadamu Sudan Kusini

Hali ya haki za binadamu nchini Sudan Kusini bado si nzuri wakati huu ambapo serikali inahaha kulinda raia dhidi ya vitendo vya ghasia,  na hiyo ni kwa mujibu wa ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa kama anavyoelezea George Njogopa.(TAARIFA YA GEORGE)

Akizungumzia hali jumla ya mambo katika eneo hilo, Naibu Mkuu wa tume

ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa Bi Flavia Pansieri amesema

kuwa baadhi ya vitendo vya uhalifu dhidi ya binadamu vimefanywa na

askari.

Amesema kuwa kuna hali ya kukatisha tama inayoendelea  inayoendelea

kujitokeza  na kwamba uhalifu zaidi umeshuhudiwa katika jimbo la

Jonglei lililopo mashariki mwa Sudan Kusin.

Katika ripoti yake kwa ofisi ya haki za binadamu Pansieri amesema kuwa

udhaifu wa vyombo vya haki na maamuzi kumesababisha kuwepo kwa

ongezeko kubwa la vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu .

Ripoti hiyo pia ilibainisha changamoto za kiusalama zinazoliandama

taifa hilo changa ambalo kwa miongo kadhaa liligubikwa na migogoro ya

wenyewe kwa wenyewe.

Akijibu kuhusu ripoti hiyo Waziri wa sheria wa Sudan Kusini John Luk

Jok amesema kuwa ni wajibu wa wananchi na vyombo vya dola kuheshimu

misingi inayozingatia haki za binadamu.