Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu milioni 1.5 wanashida ya chakula Haiti:WFP

Watu milioni 1.5 wanashida ya chakula Haiti:WFP

Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limesema linatiwa hofu na hali ya watu milioni 1.5 wanaochukuliwa kuwa na shida ya chakulaHaiti. Shirika hilo linasema kunatabiriwa kuwa na hali mbaya ya hewa hasa katika msimu huu wa vimbunga kuanzia Juni hadi Novemba na WFP inajiandaa kusambaza msaada wa chakula na kutoa msaada wa kibinadamu ikishirikiana na serikali ya Haiti na mashirika mengine ya misaada. WFP imekuwa ikitoa msaada wa dharura wa chakula kupitia mashuleni katika jamii ambazo zimeathirika saana , lakini sasa inahitaji dola milioni 17.2 ili kukidhi mahitaji.Elizabeth Byrs ni msemaji wa WFP.

(SAUTI YA ELIZABETH BYRS)