Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Dola biloni moja zahitajika kuwalisha wakimbizi wa Syria

Dola biloni moja zahitajika kuwalisha wakimbizi wa Syria

Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP linasema litahitaji dola milioni 725 zaidi kwa kipindi cha miezi sita inayokuja ili kuweza kuwahudumia mamilioni ya raia wa Syria waliolazimika kuhama makwao kutoakana na mapigano yanayoendelea nchini humo. Jason Nyakundi anaripoti.

(RIPOTI YA JASON NYAKUNDI)

WFP inasema kuwa tayari imetumia karibu dola milioni 300 kuwatafutia chakula wakimbizi wa ndani na wakimbizi wengine walio kweyne nchi majirani. WFP inasema kuwa fedha zaidi zitasaidia kununua chakula zaidi kwa hadi wasyria milioni nne waliolazimika kuhama makwao ndani mwa nchi na wengine milioni 2.6 walioavuka na kungia nchi majirani. Shirika hilo linasema kuwa linaongeza mikakati yake ndani mwa Syria ili kuweza kufikia familia zaidi hata kama hali ya usalama inazidi kuwa mbaya. Amir Abdulla ni naibu Mkurugenzi mkuu wa WFP.

(SAUTI YA AMIR ABDULLA) IANDIKE PIA TUTASOMA HUKU