Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Balozi Mahiga azungumzia Afrika na utatuzi wa migogoro

Balozi Mahiga azungumzia Afrika na utatuzi wa migogoro

Hatimaye muda wa huduma ya Ofisi ya kisiasa ya Umoja wa Mataifa kuhusu Somalia, UNPOS, umemalizika na kuanzia Jumatatu, Juni 3, ujumbe mpya wa Umoja wa Mataifa wa kuisaidia Somalia, UNSOM, utaanza majukumu yake.Balozi Augustine Mahiga ambaye aliongoza UNPOS amesema ulikuwa ni uzoefu wa kipekee na anashukuru kuwa ameweze kusongesha mchakato wa kisiasa hadi hivi sasa nchini Somalia tayari kuna serikali na bunge. Kazi inayoendelezwa hivi sasa ni kuweka taasisi na miundombinu mingine.

Katika sehemu hii ya mwisho ya mahojiano kati ya Balozi Mahiga na Assumpta Massoi wa Idhaa hii, pamoja na kuzungumzia hatma yake anazungumzia kile ambacho angaliweza kufanya bora zaidi.