Baraza la haki za binadamu kujadili Syria
Baraza la haki za binadamu mjini Geneva Jumatano wiki hii litafanya mjadala wa dharura kuhusu hali ya haki za binadamu nchiniSyrialicha ya kupingwa vikali mjadala huo na serikali za Syria,Cuba naVenezuela.
Ombi la kufanyika mkiutano utakaojadili sualahilolimewasilishwa kwa pamoja na serikali za
Turkey,Qatar na Marekani Ijumaa iliyopita. Baraza limeombwa kujadili ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaoendelea nchiniSyriana hususani mauaji ya hivi karibuni Al Qusayr.
Mwakilishi wa Qatari Bi Alya Ahmed Saif Al-Thani amesema mjadala huo ni muhimu na ni jambo la dharura kwa sababu hali inazidi kuwa mbaya huku waathirika wakumbwa walkiwa ni wanawake na watoto.
Akipinga kufanyika kwa mjadala huo mwakilishi waSyriaamesema nchi ambazo zimeomba kufanyika mkutano huo zinaipinga serikali yaSyriakwa kutoa mafunzo na msaada kwa waasi na magaidi wanaopigana nchiniSyria.