Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IOM na harakati za kudhibiti ukatili wa kingono mashariki kwa DRC

IOM na harakati za kudhibiti ukatili wa kingono mashariki kwa DRC

Wakati Umoja wa Mataifa ukiripoti kuendelea kushamiri kwa vitendo vya ukatili wa kingono huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM limeendeleza harakati zake za kuhamasisha jamii ya eneo hilo kama njia moja ya kukabiliana na ukatili huo wa kingono.IOM ambayo imeanza harakati hizo tangu mwaka 2010 baada ya hali ya amani kuzidi kuparaganyika Mashariki mwa DRC, imesema hivi sasa inajikita zaidi katika utoaji wa mafunzo hayo jimbo la Mashariki kwa maafisa polisi na wanawake wa kawaida kwa kuwa moja ya changamoto ya kuendelea vitendo hivyo ni kutokufahamu madhara ya vitendo hivyo na kushindwa kuripoti. Jumbe Omari Jumbe ni msemaji wa IOM.

(SAUTI YA JUMBE OMARI JUMBE)