Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza kuu la afya lajadili magonjwa yasiyo ya kuambukiza:WHO

Baraza kuu la afya lajadili magonjwa yasiyo ya kuambukiza:WHO

Baraza kuu ni chombo cha ngazi ya juu kabisa cha maamuzi cha WHO ambacho huweka sera za shirika na kupitisha bajeti. Msemaji wa WHO Glen Thomasi anaainisha baadhi ya ajenda zitakazojadiliwa katika kikao hicho cha 66 cha baraza la WHO.

 (SAUTI YA GLEN THOMAS)

“Miongoni mwa maswala yatakayojadiliwa ni jinsi gani ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama kisukari, maradhi ya moyo, saratani na magonjwa sugu ya mapafu.. Kingine ni ufuatiliaji wa hatua zinazopigwa na nchi katika kufikia malengo ya maendeleo ya milenia, kuongeza juhudi za kutokomeza polio, juhudi za kulinda zaidi watoto wa chanjo za magonjwa yanayozuilika, kuzisaidia nchi katika juhudi zao za kupiga hatua kuelekea huduma ya afya kwa wote na pia ajenda ya afya ya baada ya 2015”

Kikao cha barazahilola afya kinatarajiwa kuhitimishwa Mai 28.