Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatua madhubuti zichukuliwe ili kuhakiksha maisha yaliyo bora mijini:UNEP

Hatua madhubuti zichukuliwe ili kuhakiksha maisha yaliyo bora mijini:UNEP

Wakati idadi ya watu inapoendelea kuongezeka duniani, nayo idadi ya watu mijini inazidi kuongezeka. Watu zaidi wanaendelea kuhamia mijini kutafuta ajira, wakati katika takriban nchi zote zinazoendelea, miundo msingi, ikiwemo ya usafiri, nishati na makao haikupangwa ikilinganishwa na ilivyo kwenye nchi zilizostawi.

Kwa mujibu wa Shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP, hatua madhubuti zinastahili kuchukuliwa ili kuwahakikishia maisha yaliyo bora wakazi wa mijini hatua ambayo pia itachangia kuboreka kwa uchumi. Kwenye makala ya leo mwandishi wa Nairobi, Jason Nyakundi, ameangazia changamoto zinazoukumba mji mkuu wa Nairobi nchini Kenya.

(MAKALA JASON)