Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ITU na UNODC kudhibiti uhalifu wa kimtandao

ITU na UNODC kudhibiti uhalifu wa kimtandao

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kupambana na madawa ya kulevya na uhalifu UNODC kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la mawasiliano ITU linanuia kupambana na uhalifu wa kimtandao katika nchi za Afrika Mashariki kwa kutoa mafunzo kwa watumishi katika sekta ya sheria na kuanzisha mikakati endelevu ya kukomesha uhalifu huo.Akizungumza na idhaa hii mwakilishi wa Tanzania katika mkutano wa ITU unaoendelea mjini Geneva, KONI SHIRIMA amesema ITU imeamua kuchukua hatua hiyo ili kuzisaidia nchi hizo ambazo hazijapiga hatua katika teknolojia baaada ya kubaini ukosefu wa sheria za kukabili uhalifu katika mtandao unaoonekana kukuwa kwa kasi.

(SAUTI KONI SHIRIMA)