Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Misaada kwa ajili ya kukabiliana na ukame uliokikumba kisiwa cha Marshall iko mbioni:IOM

Misaada kwa ajili ya kukabiliana na ukame uliokikumba kisiwa cha Marshall iko mbioni:IOM

Shirika la kimataifa linalohusika na uhamiaji IOM, limesema kuwa shughuli za usambazaji wa misaada ya dharura kwenye maeneo yaliyokumbwa na ukame kaskazini mwa kisiwa cha Jamhuri ya Marshall inatarajia kuanza wakati wowote kuanzia sasa.

Zaidi ya wananchi 5,700 wanaishi kandoni mwa kisiwa hicho wamekubwa na ukame ulianza kujitokeza mwezi February mwaka huu baada ya kukosekana mvua za kutosha, hatua ambayo imesababisha kuwepo kwa mavuno hafifu na kunawasiwasi wa kuzuka janga la ukosefu wa maji ya kunywa.

Shirika la misaada la Marekani USAID limetokoa kiasi cha dola 100,000 kiasi ambacho kimeiwezesha IOM kutuma misaada ya usaidizi kwa serikali ya kisiwa hicho, kilichopo katikati baina ya Indonesia na Hawaii.