Ulimwengi unahitaji wakunga zaidi:UNFPA
Wakati ya kujifungua kwa mama kunatajwa kuwa kupindi kilicho hatari zaidi na cha miujiza kwa maisha ya mwanamke.
Wakunga wamechukua wajibu mkubwa katika jitihada za kupunguza hatari zinaowakumba wanawake wanapojifungua. Wakiwa na ujuzi wa juu, wakunga sasa wanaweza kukubiliana na hatari zinaowakumba akina mama na wana wajibu mkubwa wa kuyaweka maisha ya mama kuwa salama kote duniani.
Wakunga huwauguza akina mama kabla na baada ya kujifungua, wanalinda afya za watoto wanaozaliwa , wanatoa ushauri kuhusu upangaji uzazi, wanazuia maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na wanafahamu wakati wa kuitisha huduma za dharura.
Inakadiriwa kuwa wakunga walio na mafunzo na wanaopata msaada wanaweza kuokoa maisha ya zaidi ya wanawake 200,000 kila mwaka na mara kumi zaidi ya watoto kiasi hicho.