Robinson akutana na Museveni
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika nchi za Maziwa makuu Mary Robinson amekutana na kufanya mazungumzo na rais wa Uganda Yower Museveni ,mawaziri na wawakilishi wa asasi za kiraia nchini humo
Akiongea na waandishi wa habari mjini New York msemaji wa Umoja wa Mataifa Martin Nesirky amesema mazungumzo hayo yalilenga katika utekelezaji wa mkakati wa ushirikiakno wa amani na usalama kwa ajili ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, DRC
Nesirky amesema Mwakilishi huyo Maalum wa katibu Mkuu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameelekea Burundi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake katika nchi za maziwa makuu ambapo pia anatarajiwa kukamilisha ziara yake nchini Afrika Kusini.