Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashambulio mjini Mogadishu hayatukatishi tamaa: Balozi Mahiga

Mashambulio mjini Mogadishu hayatukatishi tamaa: Balozi Mahiga

Siku ya Jumapili ilikuwa ya giza nene hukoMogadishu,Somalia baada ya kuwepo kwa mfululizo wa mashambulio ya mabomu wakati huu ambapo serikali ya nchi hiyo inaendelea kushirikiana na wadau mbali mbali kuimarisha usalama ili shughuli za maendeleo ziweze kufanyika. Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Balozi Augustine Mahiga alizungumza na Joseph Msami wa Radio ya Umoja wa Mataifa ambapo pamoja na kulaani shambuliohilona kusema kuwa licha ya kuleta madhara makubwa haliwakatishi tamaa katika kutafuta amani ya kudumu hukoSomalia.

 (MAHOJIANO-BALOZI)