Mgogoro wa uchumi wachochea ukosefu wa ajira Ulaya:ILO
Mkutano wa tisa wa shirika la kazi duniani ILO kanda ya Ulaya umeanza rasmi mjini Oslo huku wito ukitolewa wa kutaka kuwepo kwa sera zinazoweza kuchangia kubuniwa kwa ajira zilizo bora.
Waziri Mkuu nchini Norway Jens Stoltenberg anasema kuwa mgogoro wa kiuchumi barani Ulaya umesababisha kuwepo kwa ukosefu mkubwa wa ajira.
Anasema kuwa Watu zaidi wanaendelea kubaki bila ajira na kusababisha hali inayotajwa kuwa ya kupotea kwa kizazi hiki. Naye mkurugenzzi mkuu wa ILO Guy Rider ni kuwa changamoto zilizo kwa sasa ni za kichumi na ajira pasipo na suluhu lolote , akitaka mkutano huo kutoa mapendekezo yatakayopelekea kupatikana kwa suluhu.
Kulingana na takwimu za hivi punde za ILO ni kwamba mgogoro uliopo umewaacha zaidi ya watu milioni 26.3 barani Ulaya bila ajira ikiwa ni milioni 10.2 zaidi tangu kuanza kwa mgogoro huo mwaka 2008.