Kuelekea kikomo cha malengo ya milenia, Tanzania yapiga hatua dhidi ya Maleria.
Zikiwa zimesalia takribani siku 1000 kabla ya kikomo cha malengo ya
Milenia mwaka 2015, Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa mapambano
dhidi ya magonjwa imepiga hatua katika kutokomeza ugonjwa wa Malaria
unaotajwa kusababisha vifo kadhaa huku idadi kubwa ikiwa watoto walio
chini ya umri wa miaka miatano.
Ungana na George Njogopa katika makala inayoangazia juhudi hizo.