Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taifa la Mongolia latakiwa kutumia fursa zilizopo kuinua uwekezaji

Taifa la Mongolia latakiwa kutumia fursa zilizopo kuinua uwekezaji

Tathmini kuhusu uwekezaji kutoka kwa shirika la biashara na maendeleo la Umoja wa Mataifa UNCTAD inayopendekeza kuwa taifa la Mongolia linastahili kutumia fursa ilizopota miaka ya hivi karibuni ya uwekezaji wa kimataifa kwenye sekta ya uchimbaji wa madini itajadiliwa na waziri mkuu wa nchi hiyo na mafisa wengine wa ngazi za juu serikalini.

Kwenye mkutano na mkurugenzi mkuu wa UNCTAD daktari Supachai Panitchpakdi waziri mkuu wa Mongolia Norovyn Altankhuyag anasema kuwa tathmini hiyo inatoa mwongozo ambao utaliwezesha taifa laMongoliakuboresha uwekezaji.

Katika ziara yake nchiniMongolia bwana Supachai alishiriki kwenye kongamamano lililohudhuriwa na washiriki 100 kutoka serikali , wafanyibishara wa kitaiafa na kimataifa, mashirika ya umma na yale ya kimaendeleo.

Wataalamu kwenye kongamnaohilowanasema kuwa taifa laMongolialimepiga hatua kubwa kuhakikisha kuwepo kwa mazingira salama ya uwekezaji.